Luke 6:20-23

Baraka Na Ole

(Mathayo 5:1-12)

20 aAkawatazama wanafunzi wake, akasema:

“Mmebarikiwa ninyi mlio maskini,
kwa sababu Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 b Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa,
kwa sababu mtashibishwa.
Mmebarikiwa ninyi mnaolia sasa,
kwa sababu mtacheka.
22 c Mmebarikiwa ninyi, watu watakapowachukia,
watakapowatenga na kuwatukana
na kulikataa jina lenu kama neno ovu,
kwa ajili ya Mwana wa Adamu.
23 d “Furahini na kurukaruka kwa shangwe, kwa sababu thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa kuwa hivyo ndivyo baba zao walivyowatenda manabii.

Copyright information for SwhNEN